Manowari ya Marekani iliyozamishwa wakati wa vita ya pili ya Dunia yapatikana
Mabaki ya manowari ya Marekani ambayo ilizamishwa wakati wa vita vya pili vya dunia yamegunduliwa nje ya pwani ya Australia.
Manowari ya USS Lexington iligunduliwa umbali wa kilomita 3 chini ya bahari karibu kilomita 800 kutoka pwani ya Australia.
Manowari
hiyo ilikuwa ilitoweka wakati wa vita vya Coral Sea, kati ya tarehe 4-8
Mei mwaka 1942. Zaidi ya wanajeshi 200 waliuawa wakati wa kuzama kwa
meli hiyo.

Jeshi
la wanamaji la Marekani lilithibitisha kuwa meli hiyo ilikuwa
imegunduliwa na kundi la kutafuta, linaloongozwa na mwanzilishi mwenza
wa kampuni ya Microsoft Paul Allen.
Picha zilionyeha mabaki ya meli hiyo yakiwa bado katika hali nzuri.
Tangazo
la kugunduliwa meli hiyo na ndege 11 kati ya 35 ilizokuwa imebeba,
lilitolewa na kampuni ya Bw Allen ya Vulcan siku ya Jumapili
Adm Harry Harris, mkuu wa kikosi cha jeshi la Marekani huko Pacific alisifu ugunduzi huo.
Vita vya Coral Sea vinatajwa kama hatua kubwa ya kuizuia Japan kuwa na ushawishi huko Pacific wakati wa vita.

Jeshi la Marekani lilisema kuwa wanajeshi 216 waliuawa wakati meli hiyo ilishambuliwa. Zaidi wa wengine 2,000 waliokolewa.
"Lexington
ilikuwa kwenye orodha yetu kwa sababu ilikuwa moja ya meli kuu
zilizotoweka wakati wa vita vya pili vya dunia," Msemaji wa Vulcan
Robert Kraft alisema.
Picha zinaonyesha majina ya Lexington na bunduki zake. Baadhi ndege za meli hiyo pia nazo zinaonekana zikiwa hali nzuri.
Meli hiyo haitaondolewa baharini kwa sababu jeshi la wanamaji la Marekani linaitaja kuwa kaburi la vita.

Bw Kraft alisema imechukua karibu miezi sita ya kupanga kupata meli hiyo.
Mwaka uliopita Vulcan ilingundua mabaki ya meli ya USS Indianapolis, ambayo ilizama mwezi Julai mwaka 1945.
Imegundua vyombo vingine vikiwemo meli ya vita ya Japan, Musashi na nyingine ya Italia Artigliere zote kutoka eneo hilo.
BB
MANOWARI YA MAREKANI YAPATIKANA
Reviewed by taragwa
on
March 06, 2018
Rating:
Reviewed by taragwa
on
March 06, 2018
Rating:

No comments: